MIAKA 51 YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR:-Rais Kikwete aungana na Watanzania kwenye Sherehe leo Jumatatu Januari 12, 2015 uwanja wa Aman ,Zanzibar.

By
Advertisement

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Jakaya Kikwete, akisalimiana na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Ali Mohammed Shein, wakati wa sherehe za miaka 51 ya Mapinduzi matukufu ya Zanzibar kwenye uwanja wa Aman, leo Jumatatu Januari 12, 2015.

Zanzibar inaadhimisha miaka 51 ya Mapinduzi, yalioung'owa utawala wa Sultani. 

Katika kilele cha maadhimisho hayo ya kushehrehekea  miaka 51 ya mapinduzi ya Zanzibar ,sherehe ambazo  zilifanyika uwnaja wa amani na kuhudhuriwa na mamaia ya waannchi na viongozi wakuu wote wa Serikali ya Muungano wa Tanzania Na Zanzibar,viongozi wastaafu  wakiongozwa na Rais wa Jamhuri Dr.Jakaya Kikwete, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa baraza la mapinduzi Dr Ali Mohamed Shein ametangaza kuondoa gharama zote za kuchangia  elimu za msingi na sekondari  na sasa huduma hizo zitatolewa Bure.

Dr. Shein amesema Serikali ndiyo sasa itakayobeba jukumu la kulipia gharama hizo  huku akisema huo ni uamuzi  sio mpya ila uliotolewa na muasisi wa Mapinduzi ,Marehemu Abeid Amani Karume.

Dr. Shein ambaye kabla ya hotuba yake , alipokea maandamano makubwa ya wananchi wa mikoa mitano ya     Zanzibar ,wafanyakazi wa SMT na SMZ na taasisi za kiserikali na binafsi na Wanafunzi wa vyuo mbali mbali vya Zanzibar pia alielezea  hali ya uchumi wa zanzibar ambapo amesema kiwngo hicho cha uchumi kiazidi kuongezeka kila mwaka sambamba na pato la Seriklai  hivyo amesisitiza utendaji  na ufanisi wa seriklai katika kuwatumikia wananchi.


JK, akisabahiananna Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Alhaj Ali Hassan Mwinyi, a.k.a "Mzee Rukhsa"
JK akisalimiana na Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar, Maalim Seif Shariff Hamad.
JK akisaliamiana na REais Mstaafu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Benjamin Mkapa, "Mzee wa uwazi na Ukweli"

JK akisalimiana na Mama Fatma Karume, mjane wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Abeid Aman Karume

JK na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Jenerali Davis Mwamunyange....

Mapema makamo wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi akitoa tathimini ya sherehe hizo, amesema jumla  ya miradi  50 imezinduliwa yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 165. 

Sherehe hizo zilizokuwa za aina yake  ambapo Rais Shein  mara alipowasili alipogiwa mizinga 21 na kukagua gwaride  la vikosi vya ulinzi na usalama vya Jamhuri ya Mungano na badaye  kulipokea gwaride la vikosi hivyo  viliyoongozwa na  Luten kanali Adam ambayo vilipita  kwa mwendo wa pole pole na badaye kupita kwa mwendo wa kasi  na baadaye  kipitakikosi cha makomandoo wa vita.

Sherehe hizo za kutimiza miaka 51 zilianza usiku wa kuamkia Jumatatu Januari 12,2015 ambapo makamu wa pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi aliongoza mamia ya waananchi katika viwanja vya maisara ambapo fash fash  zilirushwa na kuwepo kwa fataki zilizotanda usiku huo.

0 comments:

Post a Comment

Pages